Rais Bashar al-Assad amesema kuwa
ushindi wa wanajeshi wake katika mapigano mjini Aleppo utakuwa ni hatua
muhimu katika kumaliza mapigano nchini Syria.
Vikosi vyake pamoja
na washirika wake,wameleta mabadiliko makubwa mjini humo na kuwekwa
katika nafasi ya kuangamiza vikosi vya waasi vilivyosalia katika eneo
hilo.Awali katika hali isiyo ya kawaida viongozi wa nchi za magharibi, Marekani, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani waliamuru kusitishwa kwa mapigano hayo.
Wameeleza kuwa matatizo ya kibinadamu wanayoshuhudia pamoja na picha za watoto waliofariki zina vunja moyo.
Wameishutumu serikali ya Syria na muungano wao na Urusi kwa kile kilicho elezwa kuwa kikwazo kwa jitihada za misaada ya kibinadamu.
No comments:
Post a Comment