Monday 12 December 2016

Donald Trump hints US could end 'One China' policy

whether the US should continue its "One China" policy, a move likely to infuriate Beijing.
Under the policy, Taiwan, which China views as a breakaway province, is formally seen as part of the mainland.
It has been a key to US-China relations for decades, and allowed the US to keep close relations with Taiwan.
But in an interview Mr Trump said he saw no reason why that should continue without key concessions from Beijing.
His comments prompted an angry response from Chinese state media. An editorial in the Global Times warned him that the "One China policy cannot be traded".
It comes after he took a phone call from Taiwan's President, sparking a diplomatic row and a formal protest from Beijing.
It was in 1979 that the US broke formal diplomatic ties with the self-ruled island of Taiwan and switched recognition to China, ushering in a new era of deepening ties.

'Very disrespectful'

In the interview, broadcast by Fox News on Sunday, Mr Trump said: "I don't know why we have to be bound by a One China policy unless we make a deal with China having to do with other things, including trade."
Mr Trump also said China was not co-operating with the US on its handling of its currency, on North Korea, or on tensions in the South China Sea.
No US president or president-elect had spoken directly to a Taiwanese leader for decades. But in the Fox interview, Mr Trump said it was not up to Beijing to decide whether he should take a call from Taiwan's leader.
"I don't want China dictating to me and this was a call put into me," Mr Trump said. "It was a very nice call. Short. And why should some other nation be able to say I can't take a call?
"I think it actually would've been very disrespectful, to be honest with you, not taking it."
In the same interview, Mr Trump said he "doesn't believe" a CIA assessmentthat Russian hackers tried to sway the US presidential election in his favour.

'Resolute battle'

His comments prompted an angry editorial in state media outlet Global Times, known for its hawkish rhetoric.
Titled "Mr Trump please listen clearly: The One China policy cannot be traded", it labelled Mr Trump's move "a very childish rash act" and said he needed "to humbly learn about diplomacy".
It also called for a strong response, saying: "China must resolutely battle Mr Trump, only after a few serious rebuffs then will he truly understand that China and other global powers cannot be bullied."
China has so far been restrained in its official responses to Mr Trump, choosing instead to stress on the importance of Sino-US ties.
Its foreign ministry has said it would not comment on his tweets, although it has labelled the Trump-Tsai phone call a "petty trick" by Taiwan.

Outlines of a strategy? Analysis by John Sudworth, BBC News, Beijing
Well it's not as if Donald Trump didn't tell us he was going to be tough on China.
Now, though, we are getting what looks like the outline of a strategy: the use of Taiwan as a bargaining chip.
It's a bold - some would say reckless - gambit, given that for China there is nothing vaguely negotiable about the island's status.
So far, at each stage - from Mr Trump's campaign rhetoric, to his protocol-breaching phone call with the Taiwanese president - China has been measured in its response, daring to hope that it has all been based on bluster or miscalculation.
That may now begin to change, with the blow-hard state-run tabloid, The Global Times, true to form in being the first to up the ante, with the talk of retaking Taiwan by force, or of arming America's foes.
We'll know soon enough whether Beijing's official rhetoric will follow suit.

Trump akana madai kuwa Urusi ilishawishi uchaguzi

Rais mteule wa Marekani Donald Trump amesema haaminiakuwa ripoti ya CIA ambayo ilisema kuwa wadukuzi wa Urusi walijaribu kushawishi matokeo ya uchaguzi wa Marekani kwa kumpendelea.
Katika mahojiano na kitoa cha Fox News, Trump aliwalaumu wanademokratic kwa taarifa hizo zinazosema kuwa Urusi ndiyo iliendesha udukuzi huo.
Maafisa wa Urusi mara nyingi wamekana madai hayo.
Maafisa wa vyeo vya juu katika Republican sasa wamejiunga na wenzao wa Democratic wakitaka mashirika ya ujasusi kufanyiwa uchunguzi.
Kwa taarifa ya pamoja Seneta wa Republican John MacCain na seneta wa Democratic Chuck Schhumer wamesema kuwa kuwa ripoti ya CIA ni kumweka wasi wasi kila mmarekani.

Zaidi ya 30 wafariki kwenye moto wa lori lenye gesi Kenya

Idadi ya watu waliofariki katika ajali mbaya ya kuteketea kwa lori nchini Kenya, imepanda na kupita watu 30.
Kwa mjibu wa naibu kamanda mkuu wa jimbo la Nakuru Isaaca Masinde, ajali hiyo iliyotokea usiku wa kuamkia Jumapili katika eneo la Karai kwenye barabara ya kutoka Nairobi kuelekea Naivasha.
Lori moja lilianguka na kulipuka katika eneo la barabara hiyo yenye shughuli nyingi nchini Kenya na kusababisha vifo vya watu 30 papo hapo.
Watu wengine zaidi walifariki wakitibiwa mjini Naivasha.
Akihutubia waandishi wa habari hii leo, waziri wa masuala ya ndani nchini Kenya Joseph Nkaissery amesema kuwa watu 33 waliaga dunia wakimemo polisi 11 wa kikosi cha Recce ambacho humlinda rais na watu wengine mashuhuri.
Nkaisssery pia alisema kuwa sio gari la kusafirisha mafuta lililolipuka bali gari aina ya Canter lililokuwa na mitungi ya gesi inayoshika moto kwa haraka, iliyokuwa ikisafirishwa kutoka Mombasa kwenda Kampala, Uganda,.
Mtu mmoja kwa jina Moses Nandalwe aliyeshuhudia ajali hiyo, ameiambia BBC kuwa, magari kadhaa yalishika moto na kuanza kuchomeka, huku watu wengi waliofika katika eneo la ajali hiyo ili kushuhudia kilichotokea, wakikumbwa na moto huo na kisha wakachomeka.


Polisi wanachunguza chanzo cha ajali hiyo. Kuna ripoti gari aina ya Canter iligonga tuta la barabarani na kisha kuyagonga magari yaliyokuwa yakitoka upande wa mbele kabla ya kulipuka.
Miongoni mwa magari yaliyoteketea ni Basi moja la matatu lililokuwa na abiria 14, ambao wanahofiwa wote wamefariki.
Ajali hiyo mbaya imetokea nchini Kenya, wakati ambapo madaktari na wauguzi wakiendelea na mgomo wao, hatua ambayo imelemaza kabisa shughuli za matibabu katika hospitali za umma.Idadi ya watu waliofariki katika ajali mbaya ya kuteketea kwa lori nchini Kenya, imepanda na kufikia 40.

Rwanda kufanya uchaguzi wa rais Agosti, 2017

Serikali ya Rwanda imetangaza tarehe za uchaguzi wa rais unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Kulingana na tangazo la lililotolewa baada ya kikao cha baraza la mawaziri uchaguzi huo utafanyika tarehe 4 Agosti, 2017.
Shughuli za kampeni zitaanza mwezi Julai lakini hakuna tarehe rasmi iliyotangazwa kwa wagombea kuwasilisha hati za kugombea urais, licha ya kwamba tangazo hilo linasema wagombea watatangazwa kabla ya kuanza kwa kampeni.
Kwa mujibu wa katiba mpya ya rais Paul Kagame anaruhusiwa kuwania muhula wa tatu.
Mtu pekee katika kambi ya upinzani aliyetangaza nia yake ya kugombea urais ni kasisi wa zamani wa kikatoliki Joseph Nahimana. Hata hivyo juhudi zake za kutaka kurejea nchini Rwanda wiki mbili zilizopita ili kuandikisha chama chake na kugombea urais ziligonga mwamba.
Kasisi Joseph Nahimana na wenzake watatu walikataliwa kuingia nchini Rwanda walipokuwa mjini Nairobi Kenya kuelekea Rwanda kutoka nchini Ufaransa anakoishi kama mkimbizi.
Serikali ya Rwanda haikutaka kuzungumza lolote kuhusu tukio hilo, lakini mashirika ya Rwanda yanayotetea maslahi ya manusura wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 walikuwa wameanza kulalamika kuwa tovuti ya Padre Nahimana akamatwe kwa madai kwamba tovuti yake inaendeza na kuchoche fikra za mauaji ya kimbari.

Gambia: Yahya Jammeh kwenda mahakamani kupinga matokeo

Kiongozi wa Gambia Yahya Jammeh amesema atakwenda mahakamani kupinga kushindwa kwake katika uchaguzi unaoweka kikomo cha utawala wake wa miaka 22.
Awali rais Rais Jammeh alikubali kushindwa baada ya mpinzani wake Adama Barrow kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa wiki iliyopita, lakini baadae alibadilisha kauli yake Ijumaa, akisema ''anakataa kwa ujumla'' matokeo.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limemtaka akubali kushindwa.
Mitaa ya mji mkuu Banjul iko katika hali ya utulivu huku jeshi likipiga doria mjini humo.
Muungano wa Jammeh -Alliance for Patriotic Reorientation and Construction party Ulitangaza usiku wa Jumamosi , kwamba utawasilisha kesi katika mahakama kuu ya Gambia.


Kwa mujibu wa sheria za Gambia, malalamiko kuhusu matokeo yanaweza kupingwa kisheria katika kipindi cha siku 10 baada ya kupigwa kura.
Rais mteule Barrow Jumapili alisema kuwa anahofia usalama wake. Aliwahi kumshutumu Bwana Jammeh kwa kukiuka demokrasia kwa kukataa kukabidhi mamlaka.
Bwana Jammeh, ambaye alinyakua mamlaka kwa njia ya mapinduzi mwaka 1994, ameelezea kuweo kwa ''dosari'' katika upigaji kura na anataka uchaguzi urudiwe.

Saturday 10 December 2016

Bibi awa mama Uingereza

Ama kweli ,duniani kuna mambo!Mwanamke mmoja ameamua kubeba mimba, kuzaa mtoto kwa niaba ya bintiye.Mwanamke huyo jina lake ni Julie Bradford, mwenye umri wa miaka 45, alijifungua mtoto aitwaye Jack kwa niaba ya bintiye Jessica Jenkins, ambaye yuko katika matibabu ya ugonjwa wa saratani ambao umesababisha awe tasa.
Jessica, mwenye umri wa miaka 21, mwenyeji wa Rhymney, aliamua kupeleka mayai yake kugandishwa katika chuo kikuu cha utabibu cha Cardiff huko Wales kabla hajaanza matibabu yake ya saratani ya kizazi yalianza miaka mitatu iliyopita.
Jesica anasema tangu akiwa binti mdogo alikuwa na ndoto ya kuwa mama, na sasa ndoto yake imetimia, Jesica na mumewe Rees waliamua kutumia njia ya uzazi ya kupandikiza mapema mwaka huu.
Jesica aligundulika kuwa na ugonjwa wa saratani mnamo mwaka 2013, alipokuwa na umri wa miaka 18 wakati ambao madaktari waliona ni mapema mno kumuanzishia matibabu ya kansa ya kizazi .
Jesica anatoa ushuhuda kwamba madaktari walifanikiwa kuchukua mayai ishirini na moja tumboni mwake kabla ya kuanza matibabu na kati ya hayo ni mayai 10 ndiyo yaliyo nusurika yakaoteshwa kwa wiki mbili na baadaye kugandishwa, na mwezi wa tano mwaka huu yaliyeyushwa na kuwekwa tumboni mwa mamake Jesica na hivyo kumpa nafasi ya kuishi mtoto Jack na kukua tumboni mwa bibi yake.
Mamake Jesica anasema kwamba bintiye alipopewa taarifa za ugonjwa wake alijiona hana thamani tena na ndoto yake ya kuwa mama kuzimwa na saratani ya kizazi, wakati saratani ilipoondoa uwezekano wa Jess kubeba ujauzito wote tulikufa moyo.
Nikaamua kuwa nitabeba ujauzito kwa niaba yake na itakuwa fahari kuwabebea ujauzito kwa heshima ya familia ya mwanangu, tumetumia muda mwingi katika hospitali mbali mbali limekuwa jambo la kawaida kwetu. Nina furaha ya ajabu kwamba mara hii imekuwa kwa sababu maalum.

Uchaguzi Marekani: Obama ataka maswala ya udukuzi kuchunguzwa

Rais Obama ameagiza idara ya usalama nchini humo kuchunguza kwa undani maswala ya udukuzi yaliyotajwa kufanyiwa mitandao ya nchini wakati wa uchaguzi na wadukuzi wa Urusi.

Msemaji wa Ikulu ya White House alitaja uchunguzi huo kama hatua muhimu sana ya kutaka kujua uhuni wa hila ambao umekuwa ukifanywa na wadukuzi tangu mwaka 2008.
Matokeo ya uchunguzi huo yanapaswa kuwa yamekamilika kabla ya Rais Obama kuondoka mamlakani mwezi ujao.
Hata hivyo haijulikani iwapo matokeo hayo yatatangazwa hadharani.
Maafisa wa usalama wanadai kuwa Serikali ya Urusi ilipanga udukuzi katika barua pepe za chama cha Democratic.
Wanasema kuwa udukuzi huo ulikuwa na hila ya kutaka kuingilia shughuli za uchaguzi nchini humo.
Mrithi wa Bw Obama, Donald Trump, amesema kuwa hadhani Urusi iliingilia uchaguzi huo.
Mshauri wa Urais wa maswala ya usalama, Lisa Monaco amesema kuwa udukuzi si jambo geni lakini shughuli zake zimeimarika mwaka huu.

Wanasiasa wa upinzani Burundi wamkataa Mkapa

Wanasiasa wa upinzani nchini Burundi walio uhamishoni wamepinga jitihada za aliyekuwa rais wa Tanzania za kutatua mzozo ulio nchini humo.
Hii inajiri baada ya William Mkapa kuwaambia waandishi wa habari kuwa si jambo zuri kuendelea kutilia shaka uhalali wa Raia Pierre Nkurunzia.
Nchi ya Buurndi ilitumbukia kwenye mzoo baada ya bwana Nkurunziza kutangaza kuwa angewania muhula wa tatu.
Mamia ya watu wameuawa na maelfu kukimbia nchi kulipozuka ghasia.
Bwana Mkapa alipewa jukumu la kusaidia kutatua mzozo huo, na amesema kuwa makubaliano yataafikiwa ifikapo mwezi Juni mwaka ujao.
Baadhi ya wanasiasa wa upinzani walio uhamishoni wanatafutwa na serikali kwa kupanga maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza hatua ambazo serikali inazitaja kuwa za kihalifu.
Wengine waliilaumiwa wa kushiriki kwenye mapinduzi ya kijeshi yaliyofeli mwezi Mei.

Kiongozi wa upinzani ashinda uchaguzi wa urais Ghana

Kiongozi wa upinzani ashinda uchaguzi wa urais Ghana


Nana Akufo-Addo, alishangilia ushindi wake na kusema taifa hilo sasa ni mwenge wa demokrasia Afrika Magharibi.
Ameahidi kukabiliana na uchumi uliozorota, swala ambalo lilitiliwa mkazo wakati wote wa kampeni,
Bw Akufo-Addo alisema kuwa ushindi wake ni hatua anayofurahia sana katika maisha yake yote na akaahidi kuwa atafanya kila juhudi kuhakikisha kuwa anatekeleza matakwa ya wananchi wa Ghana.
Amepongezwa na mshindani wake mkuu, rais John Mahama, aliyeahidi kuheshimu matokeo ya uchaguzi.

Total Pageviews