Wednesday 30 November 2016

Watu 76 wamekufa katika ajali ya ndege COLUMBIA


Watu 76 wamepoteza maisha baada ya ndege waliokuwa wakisafiria kutoka BOLIVIA kwenda COLUMBIA kuanguka.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria 81 wakiwepo wachezaji wa klabu ya soka ya  BRAZIL imeanguka ikielekea katika uwanja wa ndege wa mji wa MEDELLIN nchini COLOMBIA.

Ndege hiyo aina ya  AEROSPACE 146 iliyokuwa inafanya safari zake kutoka BOLIVIA kwenda COLOMBIA inadaiwa kupata hitilafua kwenye mfumo wake wa  umeme.

Vikosi vya uokoaji vinaendelea kuwatafuta walionusurika igawa hali mbaya ya hewa inazuia vikosi hivyo kufika katika eneo la tukio. Hakuna moto uliowaka kwenye ndege hiyo baada ya kuanguka na kuongeza matumaini ya kupatikana kwa watu zaidi walio hai.

No comments:

Post a Comment

Total Pageviews