Rais Mteule wa Marekani Donald Trump amefanya mkutano wa kwanza wa
hadhara tangu kushinda urais ambapo amemtangaza jenerali mstaafu James
Mattis kama waziri mpya wa ulinzi.
Jenerali Mattis maarufu kama 'Mad Dog', ni mwanajeshi wa zamani aliye na
sifa ya kuweka mikakati, kuwa na msimamo mkali na mpinzani mkubwa wa
Iran.
Trump kutangaza baraza lake la mawaziri
Trump alimfananisha James Mattis na Jenerali George Patton, kamanda wa
jeshi la Marekani kwenye vita vikuu vya pili ambapo wenzake walimpa jina
la '' Old Blood-and-Guts" kutokana na ujasiri wake.
Akihutubia mkutano wa hadhara katika jimbo la Ohio, Trump ameapa kutumia
mamlaka yake kukandamiza kabisa ugaidi ndani ya Marekani
Amesema watu wasiojulikana wanaingia Marekani kutoka Mashariki ya kati na kusema atawazima kabisa.
Donald Trump afanya uteuzi wa mapema
Rais huyo mteule amesisitiza kauli yake kwenye kampeini ya kuweka
maslahi ya Marekani mbele akisema raia wa Marekani wanajali zaidi
masuala ya ndani ya nchi na siyo matukio ya kimataifa.
idha amelaani lugha ya uchochezi na mgawanyiko.
No comments:
Post a Comment